Wataalam hao hushauri hivyo kutokana na maziwa ya mama kuwa na virutubisho vyote muhimu vinavyohitajika kwenye ukuaji mzuri wa mtoto na kumpatia kinga ya magonjwa mbalimbali.
Hivyo hii leo Mandai Herbalist Clinic inayofuraha
kukufahamisha wewe mzazi namna ya kuanza kumpatia mtoto wako chakula mara
anapofika miezi 6 pamoja na faida za lishe bora kwa mtoto wako.
Mtoto anapoanza kupewa vyakula
vingine zaidi ya maziwa ni lazima vipondwa vizuri, au viwe kwenye mfumo wa uji
au maji sababu mtoto anakuwa hana meno yaliyokomaa na watoto wengine huwa wanakuwa
hawajaanza kabisa kuota meno.
Pia inatakiwa kuzingatiwa kuwa,
vyakula vya mtoto viwe vya kuongezea lishe, hata hivyo, ni vizuri mtoto akaendelea
kunyonya maziwa ya mama hadi atakapofikisha miezi 24.
Hii ni kwa sababu maziwa ya mama ni
muhimu katika kumfanya mtoto akue vizuri, hasa katika miezi 24 ya mwanzo.Hivyo
endapo hakuna vikwazo vyovyote inashauriwa kuwa mtoto aendelee kunyonya.
Vikwazo hivyo vinaweza kuwa ugonjwa wa maambukizi unaoweza kumdhuru mtoto.
Hata hivyo, ni vizuri zaidi mama akimnyonyeshe
mtoto kwa muda mrefu zaidi ya miezi sita, kwani kuna faida kubwa za kufanya hivyo kwa mtoto, ambazo ni pamoja na kumsaidia ubongo wake kukua vizuri zaidi sababu maziwa ya mama yanatoa
virutubisho kwa wingi kuliko vyakula atakavyokula yeye moja kwa moja na hii ni
kwa sababu kubwa.
Lakini pia ni vizuri ufahamu kuwa tumbo la mtoto huwa halijazoea kusaga vyakula tofauti,
hivyo maziwa ya mama ni chakula kinacholeta virutubisho vinavyotumika moja kwa moja
mwilini mwa mtoto.
Endapo mtoto atakosa lishe bora basi
atakuwa akipata magonjwa mara kwa mara sababu ya kukosa kinga imara dhidi ya
magonjwa pia kudumaa kwa akili na mwili.
pamoja na madhara mengine yanayoweza
kujitokeza ni uwezekano mkubwa wa kupata ulemavu sababu mifupa kwani inakuwa laini na
haiwezi kustahimili uzito wa mwili, hali kadhalika na hata kupata utapiamlo au mtoto kupoteza maisha
katika umri mdogo.
Mandai Herbalist Clinic tunapatikana Ukonga, Mongolandege jijini Dar esa Salaam na tunatoa tiba ya magonjwa mbalimbali.
No comments:
Post a Comment