
Ikiwa bado watanzania hawajasahau majonzi ya kumpoteza Mwenyekiti wa DP Mchungaji Christopher Mtikila aliyezikwa jana, leo tena kwenye siasa kuna majonzi mengine ambapo Mgombea mwingine wa Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa Tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Estomih Mallah amefariki Dunia baada ya kuugua na kukimbizwa Hospitali.
Taarifa ya kwanza ilisema kuwa Mgombea huyo amefariki katika Hospitali ya KCMC Moshi ambapo alikuwa akipatiwa matibabu… Nimempata Msemaji wa Chama cha ACT-Wazalendo, Khamis Abdallah amenifikishia taarifa nyingine kuhusu Kifo cha Mgombea huyo.
“Tatizo lilianza October 06 2015 wakati anajiandaa kwenda kwenye Mkutano wa Mgombea Urais, alisema anajisikia vibaya kichwa kinamuuma… Hakuweza kupanda Jukwaani, akapelekwa Hospitali ya KCMC baada ya hali kuwa mbaya. Jana saa nane usiku tukatumiwa taarifa ya msiba.”
Chanzo: Millard ayo.com
No comments:
Post a Comment