Marehemu Akwilina Akwilini
MWILI wa marehemu Akwilina Akwilini aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha
Usafirishaji (NIT), Dar es Salaam unatarajiwa kusafirishwa hadi Rombo, mkoani
Kilimanjaro kwa mazishi.
Wazazi wa marehemu walipata taarifa za kifo cha mwanafunzi huyo
Ijumaa baada kuuawa kwa kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa ni polisi baada
ya makabiliano kati yao na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Ndugu wa marehemu Damiani Swai amesema watachukua hatua baada ya
matokeo ya uchunguzi kutoka Jeshi la Polisi ambalo linaendelea nao sasa.
Mwanafamilia huyo amesema Akwilini alikuwa na ndoto za kufika
mbali kielimu lakini zimezimwa akiwa katika harakati za kuzifikia.
Serikali kupitia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Prof.
Joyce Ndalichako imesema itagharamia mazishi ya mwanafunzi huyo.
Hadi wakati huu taarifa zilizo ni kwamba polisi sita wanaendelea
kuhojiwa kutokana na kifo cha mwanafunzi huyo.
Kumekuwa na shinikizo kutoka vyama vya upinzani kikiwemo ACT
Wazalendo, vijana na Shirika la wanafunzi nchini kumtaka waziri wa Mambo ya
Ndani Mwigulu Nchemba kujiuzuru nafasi hiyo baada ya kisa hicho cha
kusikitisha.
No comments:
Post a Comment