Udongo mweusi
YUTIKARIA ni ugonjwa wa kuwashwa na kuwa na uvimbe mwili mzima. Mara nyingi ugonjwa wa aina hii ni dalili ya mzio.
YUTIKARIA ni ugonjwa wa kuwashwa na kuwa na uvimbe mwili mzima. Mara nyingi ugonjwa wa aina hii ni dalili ya mzio.
Mwathirika anapata uvimbe ghafla na kuwashwa na
kisha hali hiyo huweza kutoweka ghafla licha ya kuwa wakati mwingine inaweza
kudumu kwa muda mrefu na hivyo kuhitaji tiba.
Zipo tiba nyingi za asili miongoni mwanzo ni udongo
mweusi, tui la nazi na mtindi, maji ya mchele, ndimu, asali na bizari.
Udongo mweusi
Paka udongo mweusi mwili mzima na baada ya saa moja
oga ili kuondoa udongo wote
Tui la nazi
Baada ya kuoga, paka tui la nazi au mtindi mwili
mzima. Baada ya saa moja oga mwili mzima.
Maji ya mchele
Pia unaweza kunywa maji yaliyooshewa mchele,
asubuhi na jioni kwa muda wa siku tatu. Hakikisha maji uliyoshea ni safi na
salama.
Ndimu na asali
Changanya juisi ya ndimu na asali, ongeza maji ya
kawaida nusu glasi, halafu kunywa. Fanya hivyo asubuhi na jioni kwa muda wa
siku tatu.
Bizari
Kula kikonyo kimoja cha bizari kila siku asubuhi,
kabla ya kupata kifungua kinywa kwa muda wa siku tano.
Mchanganuo huu umeletwa kwako na Mtaalamu wa tiba, lishe na virutubisho,
Abdallah Mandai.
Yeyote anayesumbuliwa na tatizo la kiafya na ushauri, karibu makao
yetu makuu, Ukonga Mongolandege, Dar es Salaam au awasiliane na Mtaalam Mandai
kwa ushauri na kujipatia virutubisho mbalimbali vinavyoukinga mwili dhidi ya
magonjwa.
Mtaalamu Mandai anapatikana kwa simu +255745900600 au
barua pepe dkmandaitz@gmail.com.
No comments:
Post a Comment