Marehemu Dk. Amani Kabourou
ALIYEWAHI kuwa mbunge wa Kigoma
Mjini, Dk. Amani Kabourou amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali
ya Taifa Muhimbili alikokuwa anapatiwa matibabu.
Dk. Kabourou ambaye aliwahi
kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amefariki
akiwa na umri wa miaka 79, alizaliwa mwaka 1949.
Wakati wa uhai wake licha
ya kuwa mbunge wa Jamhuri, pia alikuwa mbunge wa Bunge la Afrika Masharikia,
kati ya mwaka 2007 hadi 2012 pia alikuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi
(CCM), mkoa wa Kigoma baada ya kuhama Chadema.
Mbunge wa sasa wa Kigoma
mjini, Zitto Kabwe amesema kupitia ukurasa wake wa facebook kuwa huo ni msiba
mkubwa kwa wananchi wa jimbo hilo na Watanzania kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment