Robert Mugabe
ALIYEKUWA Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amevunja ukimya kwa mara ya
kwanza tangu aondolewe madarakani, amesema amekua muhanga wa mapinduzi ya
kijeshi.
Akizungumza na televisheni
ya SABC ya Afrika Kusini, Mugabe amesema Rais wa sasa Emerson Mnangagwa
asingeweza kuingia madarakani bila jeshi kuingilia kati.
Akiwa katika nyumba
yake ya kifahari mjini Harare, Mugabe amekemea mbinu zilizotumika kumuondoa
madarakani.
Amesema alikuwa tayari
kufanya mazungumzo na Rais wa sasa Emerson Mnangagwa na angehakikisha
mabadiliko ya madaraka ya uhalali na si yale ya kulazimishwa.
Mugabe amesema kuwa
yuko tayari kwa ajili ya mazugumzo na Mnangagwa ili kulinda katiba yao.
Hakuna uhakika kama
rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 94 iwapo anataka kurudi madarakani ama
la, lakini ni wazi kuwa anadhani amesalitiwa na Mnangagwa rais wa sasa wa taifa
hilo.
Amesema hakudhani kama
angepoteza imani yake kwa Mnangagwa kwani yeye ndiye alimsaidia kuingia
serikalini.
“Siamini kama yeye
Mnangagwa angeweza kuniondoa madaraki , nimemuingiza serikalini, nimemsaidia
alipokua jela anataka kunyongwa, sikuwaza kabisa kama siku moja ndiye atakuwa
mtu wa kunitoa madarakani,” amesema Mugabe.
Aidha, Mugabe ameongeza
kuwa Rais Mnangagwa ameingia madarakani kwa njia zisizo halali.
“Lazima tufute aibu
hii, ambayo tumejiletea wenyewe, hatuistahili, hatuistahili, hatuistahili ,
tafadhali hatuistahili kabisa.Tunatakiwa kuwa nchi inayoheshimu katiba, ndiyo
tunaweza kuwa na mapungufu hapa na pale lakini bado lazima tuheshimu sheria,”
amesema Mugabe.
Katika mitandao
mbalimbali ya kijamii, baadhi ya wazimbabwe wanashangazwa na mkongwe huyo wa
miaka 94 kutoa kauli huku wengine wanaamini kuwa amepoteza uhalisia kabisa
baada ya kuongoza kwa miaka 38 , wakati wake sasa umekwisha.
No comments:
Post a Comment