Kansela wa Ujerumani Angela Merkel
UJERUMANI
inasubiri kwa hamu matokeo ya uamuzi wa chama cha Social Democrats (SPD),
kuhusu iwapo wanachama wake wataridhia chama hicho kijiunge kwa mara nyingine
tena katika serikali ya mseto na chama cha Kansela wa Ujerumani Angela Merkel
cha Christian Democratic Union CDU na chama ndugu cha Christian Social Union
CSU.
Kura
ya hapana kutoka kwa SPD, miezi mitano tangu uchaguzi mkuu wa Septemba 24,
huenda ukalitumbukiza taifa la Ujerumani ambalo ndilo imara zaidi kiuchumi
barani Ulaya katika mzozo zaidi wa kisiasa.
SPD
inatarajiwa kutangaza uamuzi uliofikiwa na wanachama wake zaidi ya 460,000
mwendo kwenye makao makuu ya chama hicho yaliko mjini Berlin.
Iwapo
CDU/CSU na SPD vitashindwa kuunda serikali, basi Merkel huenda akalazimika
kuongoza serikali iliyo ya wachache au uchaguzi mpya kuitishwa.
Chanzo:
DW
No comments:
Post a Comment