Vig
Vigogo waliokutana kujadili mgogoro wa ardhi Kia wakiangalia ramani ya wanavijiji.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi),
Selemani Jafo amekutana na mawaziri wa Ujenzi na Ardhi kutafuta suluhu ya
mgogoro wa ardhi baina ya wananchi na mwendeshaji wa Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia), Kampuni ya Kadco.
Jafo amekutana jana na Waziri wa Ujenzi,
Mawasiliano na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa na Naibu Waziri wa Ardhi, Angelina
Mabula kujadili mustakabali wa mgogoro huo uliodumu karibu miongo mwili.
Mgogoro huo unahusisha zaidi ya kaya 1,200
zilizopo katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha zinazotakiwa kupisha upanuzi wa
uwanja huo.
Kaya hizo zipo katika vijiji
vilivyopimwa kisheria lakini maeneo ya vijiji hivyo yanaingiliana na eneo la
uwanja wa Kia na hivyo kusabisha mgogoro baina ya menejimentinti ya uwanja
huo na wananchi hao.
Hali hiyo ilipelekea kuundwa timu ya ufuatiliaji
na utafutaji wa suluhu ya mgogoro huo ambayo inaundwa na wizara tatu za
Tamisemi, Ujenzi na ya Ardhi wakuu wa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha na
wataalamu kutoka katika sekta mbalimbali za ardhi na mawasiliano ya anga.
Kikao hicho kilimalizika kwa kuazimia kuwa
vijiji hivyo vifanyiwe uthamini upya ili wananchi wa maeneo hayo walipwe fidia
ili kuacha maeneo hayo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanja cha ndege.
Kwa pamoja viongozi hao wamekubaliana
kuanza mchakato wa kufuta hati za vijiji hivyo na kuanza mchakato wa
kuwaelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa
eneo hilo kwa maslahi mapana ya taifa.
Mgogoro kati ya wananchi wanaozunguka
uwanja wa ndege wa Kia na kampuni ya Kadco umekuwepo tangu mwaka 1998.
No comments:
Post a Comment