Aliko Dangote
BWANYENYE
kutoka Nigeria, Aliko Dangote ndiye mtu mweusi aliye tajiri zaidi duniani kwa
mujibu wa jarida la Forbes.
Kati
ya watu 2,043 ambao wameorodheshwa kuwa mabilionea duniani katika orodha ya
Forbes ya mwaka huu, ni watu 10 pekee ambao ni weusi.
Dangote
amehifadhi taji la kuwa mtu mweusi tajiri zaidi duniani akiwa na utajiri wa
takriban dola za Marekani bilioni 14.1.
Anafuatiwa
na Mnigeria mwenzake Mike Adenuga ambaye utajiri wake unakadiriwa kuwa dola za
Marekani bilioni 5.3
Tajiri
anayejihusisha na ujenzi ambaye ana uraia wa Saudi Arabia na Ethiopia Mohammed
Al-Amoudi ambaye alikuwa na utajiri wa dola bilioni 8.4 aliondolewa kwenye
orodha hiyo mwaka huu baada ya Forbes kuamua kuwaondoa mabilionea kutoka Saudi
Arabia kwenye orodha hiyo.
Raia
wa Zimbabwe aliyewekeza katika sekta ya mawasiliano, na ambaye hutoa fedha nyingi
kwa hisani, Strive Masiyiwa, amejiunga na orodha ya watu weusi walio
mabilionea. Ndiye mtu wa kwanza kutoka Zimbabwe kuwa bilionea.
Binti
wa aliyekuwa rais wa Angola, Isabel dos Santos, Mmarekani anayejihusisha na
vyombo vya habari Oprah Winfrey na tajiri wa mafuta kutoka Nigeria Folorunsho
Alakija bado ndio wanawake pekee weusi kwenye orodha ya mabilionea duniani, kwa
mujibu wa jarida hilo.
Marekani
ndiyo nchi iliyo na mabilionea wengi duniani, ambapo ina mabilionea 585,
ikifuatwa na China. Jimbo la California pekee lina mabilionea 144, zaidi
kushinda mataifa yote isipokuwa Marekani na China.
Ujerumani
ndiyo nchi inayoongoza Ulaya ikiwa na mabilionea 123. India ina mabilionea 119
nayo Urusi mabilionea 102. Kuna mabilionea 53 kutoka Uingereza kwa mujibu wa
Forbes na idadi hiyo imeshuka kutoka 54 mwaka 2017.
No comments:
Post a Comment