Mtaalam wa tiba, lishe na virutubisho, Abdallaha Mandai akisisitiza jambo wakati akizungumzia umuhimu wa jamii kuchukua tahadhali dhidi ya vidonda vya tumbo akiwa ofisini kwake makao makuu Ukonga, Mongo la Ndege, Dar es Salaam.
VIDONDA
vya tumbo ni miongoni magonjwa tishio yanayowakumba watu wengi na hivyo kuwafanya
muda mwingi wahangaikie tiba badala ya kufanya kazi za kuwaongezea kipato
katika familia na taifa.
Kulingana
na tafiti inaonesha kuwa mtu mmoja kati 10 atakuwa anaugua vidonda vya tumbo
licha ya kuwa tafiti nyingine zinabainisha kuwa miongoni mwa watu watano mmoja
ameathirika na maradhi hayo.
Mtaalam
wa tiba, lishe na rutubisho, Abdallah Mandai anasema vidonda vya tumbo
vimegawanyika katika sehemu kuu mbili, vidonda vya ndani ya tumbo au sehemu ya
juu ya utumbo mdogo.
Vidonda
vinavyotokea katika utumbo ndiyo maarufu zaidi ambavyo huwapata zaidi wanaume
na vidonda vya ndani ya tumbo huwashambulia wote wanaume na wanawake.
Mtaalam
Mandai anasema chanzo cha ugonjwa huo ni baada ya chakula kinapoingia tumboni
ili kusagwa, tumbo huzalisha majimaji ya aina mbalimbali yakiwemo ya asidi
ambayo hufahamika kama saidi hidrokloriki.
"Asidi
hii huanza kula kuta za tumbo aina zote mbili za vidonda vya tumbo hutokea
kutokana na kutolingana nguvu kati ya nguvu ya mnyunyizo wa asidi ya tumbo
katika kushambulia na uwezo wa kuta za tumbo katika kuzuia mashambulizi," anasema.
Tabibu
huyo aliyepata uzoefu kutoka katika nchi kadhaa za Afrika, anasema kutokea
vidonda vya tumbo kunategemea zaidi vipengele viwili.
"Kwanza,
vitu ambavyo vinaongeza mnyunyizo wa asidi katika tumbo, mfano vyakula vya
kusisimua, vya mafuta, uvutaji sigara, utumiaji wa pombe, chai, kahawa na
baadhi ya dawa kama corticostisteroids, caffeine na reseprine.
"Pili,
udhaifu wa ute na kuta za tumbo kuzuia ushambuliaji wa asidi. Katika kutibu
vidonda vya tumbo, mara nyingi ni lazima kuongeza kinga ya ute au kupunguza
uzalishaji wa asidi," anasema.
Mandai
anatanabaisha kuwa mfadhaiko wa akili utokanao na shida za maisha ni moja ya
vipengele vinavyosababisha vidonda vya tumbo.
Anafafanua
kuwa mfadhaiko huo unaongeza utiririkaji wa asidi ndani ya utumbo. Hii asidi ya
ziada ambayo hutiririka ndani ya tumbo imetengenezwa kwa ajiri ya kukisaga
chakula chochote haraka iwezekanavyo.
"Lakini
kama hakuna chakula cha kufanyiwa kazi, asidi hii humomonyoa kuta za tumbo na
hivyo kusababisha vidonda.
"Utafiti
uliofanywa katika miaka ya hivi karibuni
umeonesha kuwa akili hutumia nguvu nyingi katika mwili. Baadhi ya madaktari
wamesema mfadhaiko huchangia sana kutokeza magonjwa," anasema.
Aidha,
anataja dalili tisa za ugonjwa huo kuwa ni pamoja na kujisikia huzuni kupita
kiasi hadi kupoteza matumaini yoyote, kupoteza kabisa uwezo wa akili kufurahi,
kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa na pia kutokuwa na hamu ya kula ya chakula.
Anasema
dalili nyingine ni mtu kukosa usingizi, wasiwasi unaosababisha hali ya
kutotulia pamoja, kushindwa kukumbuka na kuamua, kukasirishwa na vitu vidogo,
kujiona hana thamani na kujitenga na marafiki au ndugu.
Mtaalam
Manda anasema watu waepuke uvutaji sigara, matumizi ya dawa bila ushauri wa
wataalamu wa tiba kwa kuwa zipo zenye kemikali zinapotumiwa bila mpangilio
unamweka mtumiaji katika hatari ya kupata magonjwa.
Aidha,
anasisitiza wanajamii kuzingatia mlo kwani njaa ya muda mrefu inamweka mtu
katika hatari ya kupata ugonjwa huo.
"Mwito
wangu tu kwamba mtu asitumie dawa bila maelezo kutoka kwa wataalam kwa sababu
baadhi zina kemilika zinapotumiwa bila ushauri zinaweza kumweka mtu katika
uwezekano wa kupata vidonda vya tumbo.
"Pia
mvutaji wa sigara anaweza kupata ugonjwa huu, tena sigara inasababisha magonjwa
mengi hata TB hivyo wavutaji waache kuvuta sigara," anasisitiza.
Kwa anayesumbuliwa na tatizo lolote la kiafya
karibu makao yetu makuu, Ukonga Mongolandege, Dar es Salaam au wasiliana na
Mtaalam Mandai kwa simu
+255745900600 au barua pepe dkmandaitz@gmail.com ili kupata ushauri
au virutubisho vinavyozalishwa na kampuni yetu.
No comments:
Post a Comment